Yule kijeba aliyekutana na Simba asaka klabu ya 20
Hivi unawakumbuka wale Al Masry waliokuja kucheza na Simba mwaka jana? Sasa kuna jamaa wao yule kijeba pande la mtu miraba kama 7 hivi Aristide Bance.
Yule Bance mpaka sasa yupo pale pale Al Masry lakini inasemekana anataka kwenda klabu ya Horoya FC. Ikumbukwe mwaka jana alisema timu nyingi za waraabu hasa hasa ligi ya Misri inatisha kwa ubaguzi na kuwanyanyasa wachezaji weusi.
Bance alidai kuwa sababu kubwa wamisiri kufeli kombe la dunia ni kutokana na laana ya ubaguzi waliyo nayo kwenye ligi. Sababu hii imemfanya mchezaji asake timu ya kwenda msimu huu.
Bance ni mzaliwa wa Ivory Coast lakini ana uraia wa Burkina Faso kwa sasa. Bance ana undugu na yule nyota wa zamani wa Ivory Coast Aruna Dindane.
Rekodi kubwa ya huyu mwanaume ni kucheza vilabu vingi. Bance amecheza takribani vilabu 20 akiwa na umri wa miaka 34. Kwa sasa anasaka klabu ya 21. Na bado anasema anataka kucheza hata mpaka miaka 40.
Bance alianza kucheza soka la kulipwa 2000 katika klabu ya Stade d’Abbidjan. Ameichezea timu ya taifa ya Burkina Faco tokea 2003 michezo 73 na kufunga magoli 22. Tokea 2006 hakuwahi kuchezea timu kwa zaidi ya misimu miwili.
| Wasifu | |||
|---|---|---|---|
| Msimu | Klabu | M | G |
| 2000 | Stade d’Abidjan | 33 | (8) |
| 2001 | Athlétic Adjamé | 30 | (5) |
| 2002 | RFC Daoukro | 20 | (8) |
| 2002–2003 | Santos Burkina | 16 | (9) |
| 2003–2006 | Lokeren | 77 | (27) |
| 2006–2008 | Metalurh Donetsk | 12 | (2) |
| 2007–2008 | Germinal Beerschot (mkopo) | 9 | (0) |
| 2008 | Kickers Offenbach (mkopo) | 10 | (4) |
| 2008–2010 | 1. FSV Mainz 05 | 62 | (24) |
| 2010–2012 | Al-Ahli Dubai | 7 | (2) |
| 2011 | Umm-Salal (Mkopo) | 8 | (4) |
| 2011 | Samsunspor (Mkopo) | 20 | (5) |
| 2012–2014 | FC Augsburg | 18 | (0) |
| 2013–2014 | Fortuna Düsseldorf (mkopo) | 10 | (2) |
| 2014 | HJK Helsinki | 4 | (1) |
| 2015 | Irtysh Pavlodar | 11 | (2) |
| 2015–2016 | Chippa United | 14 | (3) |
| 2016 | Riga | 8 | (1) |
| 2016–2017 | ASEC Mimosas | 26 | (13) |
| 2017–2018 | Al-Masry | ||
from ShaffihDauda http://bit.ly/2TYD8RT
ILI KUWA WA KWANZA KUPATA HABARI USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON