YANGA SC YAICHAPA NAMUNGO FC 2-0 DAR
MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Yanga SC leo yamefungwa na beki wa Kimataifa wa Tanzania, Dickson Job dakika ya 43 na kiungo Mburkinabe, Stephane Aziz Ki dakika ya 51.
Kwa ushindi huo timu ya Wananchi inafikisha pointi 59 na kuendelea kuongoza ligi kwa pointi sita zaidi ya mtani, Simba baada ya wote kucheza mechi 22.
Kwa upande wao Namungo FC baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao 29 za mechi 22 pia nafasi ya sita.
Kwa upande wao Namungo FC baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao 29 za mechi 22 pia nafasi ya sita.
Chanzo: BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
ILI KUWA WA KWANZA KUPATA HABARI USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON
