YANGA SC WAWANYAMAZISHA SIMBA SC MBELE YA RAIS MAMA SAMIAH, WAICHAPA 1-0 BAO PEKEE LA ZAWADI MAUYA

VIGOGO, Yanga SC wamezima kelele za watani wao wa jadi, Simba SC baada ya kuwachapa bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Kwa matokeo hayo, Yanga SC inafikisha pointi 70 katika mchezo wa 31, ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi tatu na mabingwa hao watetezi kwa kwa misimu sasa, Simba SC ambao pia wana mechi mbili mkononi.
Ikumbukwe Simba ilihitaji sare tu kutawazwa rasmi kuwa mabingwa wa Ligi Kuu kwa msimu wa nne mfululizo na sasa watalazimika kusubiri hadi mechi ijayo baada ya watani kukataa kuwa ngazi ya ubingwa wao mwingine. 
Katika mchezo huo uliohudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, bao pekee la Yanga limefungwa na kiungo Zawadi Mauya dakika ya 11 kwa shuti la umbali wa mita 21 baada ya kupokea pasi ya kiufundi ya kiungo mwenzake, Feisal Salum ‘Fei Toto’.


Chanzo: BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
ILI KUWA WA KWANZA KUPATA HABARI USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON