Guardiola mtoto aliyezaliwa na meno
Jana ilikiwa siku yako muhimu na kwa kufanikiwa kuongeza mwaka mwengine kwa Pep.
Pep hilii sio geni sana masikioni mwa wapenda soka na machoni mwawatu wengi. Pep ni raia wa spain aliyefanikiwa kucheza FC BARCELONA katika kipindi chake chote cha uchezaji na kafanikiwa kushinda makombe kadhaa akiwa kama mchezaji wa FC Barcelona.
Pep ana histora fupi sana lakini yenye mafanikio makubwa sana
Pep hawezi kuondoka kichwani mwa Messi na Pep hawezi kumsahau Messi. Huyu ndie aliyeanikiwa kutuletea bidhaa adhimu iliyo tikisa ulimwengu kwa miaka takribani 13.
Pep ni mtu wa misimamo katika kipindi cha ukocha FC Barcelona. Aliamua kumuuza Ronaldinho ili kumpa muda wa kutosha Messi, kila mtu na dunia ilimshangaa. Lakini hatukujua anawaza nini.
Baada ya miaka minne ya pep akiwa na FC Barcelona aliweza kushinda mataji yote ya ngazi ya vilabu na kufanikiwa kuchangia mafanikio makubwa yaliyo patikana World cup 2010. Asilimia kubwa yakikosi cha Hispania kilijawa na vijana muhimu wa Pep
Pep aliamua kubadili changamoto na kwenda Ujerumani. Alifanikiwa kutwaa mataji kadhaa na Bayern.
Kisha akaelekea kwenye ligi ngumu ya EPL. Akatua klabu ya Manchester City. Alipigana sana lakini kwa msimu wa kwanza ilionekana ligi itamshinda na atafukuzwa kabla ya mkataba.
Msimu wake wa pili akiwa na Man City alibeba ubingwa huo. Bado anaendeleza dozi katika ligi. Kwa sasa yupo nafasi ya pili katika msimamo nyuma ya Liverpool, huu ukiwa msimu wake wa 3 katika ligi.
Aziz Mtambo
from ShaffihDauda http://bit.ly/2HnPAcr
ILI KUWA WA KWANZA KUPATA HABARI USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON