MAKAMU WA RAIS TFF, ATHUMANI NYAMLANI ALIPIKWENDA KUMFARIJI MCHEZAJI WA POLISI, ATHANAS MDAMU ALIYEUMIA AJALINI MOSHI

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Athumani Nyamlani (katikati) akimjulia hali mchezaji wa Polisi Tanzania, Athanas Mdamu kwenye Hospital ya KCMC, Moshi mkoani Kilimanjaro ambako amelazwa akipatiwa matibabu kufuatia kuumia kwenye ajali ya Basi la timu yake wiki mbili zilizopita mkoani humo.

Wengine alioongozana naye ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka Kilimanjaro (KRFA), Robert Munisi (wa kwanza kushoto) na Mwenyekiti wa Chama cha Matabibu wa Wanamichezo (TASMA) mkoani Kilimanjaro, Dk Daud Mavura ( wa kwanza kulia).


Chanzo: BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
ILI KUWA WA KWANZA KUPATA HABARI USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON