KOCHA MSAIDIZI WA SIMBA SC, SULEIMAN MATOLA NA KOCHA WA YANGA B, SAID MAULID WAENDA KUONGEZA ELIMU NA UJUZI WA KUFUNDISHA SOKA DARASANI
KOCHA Msaidizi wa Simba SC na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Suleiman Abdallah Matola (kulia) akiwa darasani katika Kozi ya Ukocha ya Diploma B ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) iliyofunguliwa leo mjini Morogoro. Kushoto ni kocha wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Yanga, Said Maulid Kalikula.
Kocha wa makipa wa timu za taifa, Manyika Peter pia ni mmoja wa washiriki wa Kozi hiyo ya miezi mitatu inayojumuisha jumla ya makocha 25 wa klabu mbalimbali za Ligi Kuu na Daraja la Kwanza Tanzania Bara.
Chanzo: BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
ILI KUWA WA KWANZA KUPATA HABARI USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON


