Raia wa Ethiopia wakimbilia Sudan kuepuka mapigano Tigray


Maafisa nchini Sudan wamesema takriban raia wa Ethiopia 6,000 wamewasili nchini humo, wakikimbia mapigano jimboni Tigray.

Mamlaka za Sudan zinajiandaa kupokea zaidi watu 200,000 watakaovuka mpaka siku za usoni.

Kambi ya wakimbizi kuhimili idadi kubwa ya watu inaandaliwa, huku taasisi za misaada zikitahadharisha kutokea kwa changamoto ya hali ya kibinadamu

Waziri Mkuu wa Ethiopia alizanzisha operesheni ya kijeshi huko Tigray dhidi ya viongozi wa eneo hilo ambao walioanzisha mzozo dhidi ya mamlaka ,za serikali.

Mamia wameuawa kwenye mapigano hayo.



Chanzo MUUNGWANA BLOG
ILI KUWA WA KWANZA KUPATA HABARI USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON