Vurugu za baada ya uchaguzi zashika kasi Ivory Coast


Kuna Ripoti za kutokea kwa vurugu za baada ya uchaguzi nchini Ivory Coast baada ya Rais Alassane Ouattara kuchaguliwa tena kwa muhula wa tatu.

Watu watatu wameuawa na wengine kujeruhiwa siku ya Jumanne katika eneo la ngome ya upinzani kwa mujibu wa mamlaka za eneo hilo wakinukuliwa na mashirika ya habari.

Mapigano yaliripotiwa maeneo ya mji wa M’Batto ulio Kusini –kati ambao umeonekana kuwa ngome ya upinzani kwa mgombea wa upinzani Pascal Affi N’Guessan, ambaye alikamatwa siku ya Ijumaa.

Bw. N’Guessan anakabiliwa na mashtaka ya ugaidi na uhaini baada ya kupinga ushindi wa Rais Ouattara.

Rais Ouattara amemualika mpinzani wake, Rais wa zamani Henri Konan Bédié kwa mazungumzo baada ya kutokea vurugu.

Bw.Bédié hajazungumza lolote kuhusu mualiko huo.






Chanzo MUUNGWANA BLOG
ILI KUWA WA KWANZA KUPATA HABARI USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON